INJILI ULIMWENGUNI - SEHEMU YA NANEنموونە

KUJIGEUZA KWA YESU
28 Yapata siku nane baada ya Yesu kusema hayo, aliwachukua Petro, Yakobo na Yohana akaenda nao mlimani kuomba.
Alipokuwa akiomba, mwonekano wa sura yake ukabadilika, mavazi yake yakametameta kama mwanga wa umeme wa radi.Ghafula wakawaona watu wawili, Mose na Eliya wakizungumza naye.Walionekana katika utukufu wakizungumza na Yesu kuhusu kifo chake ambacho kingetokea huko Yerusalemu.
32 Petro na wenzake waliokuwa wamelala usingizi mzito walipoamka,
wakaona utukufu wa Yesu na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33 Mose na Eliya, walipokuwa wanaondoka, Petro akamwambia Yesu,
“Bwana, ni vizuri tukae hapa! Tutajenga vibanda vitatu, kimoja chako, kingine cha Mose na kingine cha Eliya.” Lakini Petro alikuwa hajui asemacho.
34 Alipokuwa bado anazungumza, pakatokea wingu likawafunika, nao wakaogopa walipoingia mle kwenye wingu.Sauti ikatoka kwenye lile wingu ikisema,
“Huyu ni Mwanangu mpendwa niliyemchagua, msikilizeni yeye.”
36 Baada ya sauti hiyo kusema, walimkuta Yesu akiwa peke yake.
Wale wanafunzi wakalihifadhi jambo hili, wala kwa wakati huo hawakumwambia mtu ye yote yale waliyokuwa wameyaona.
کتێبی پیرۆز
دەربارەی ئەم پلانە

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana
More
پلانە پەیوەستەکان

How to Become a Real Disciple

Film + Faith - Superheroes and the Bible

Stop Living in Your Head: Capturing Those Dreams and Making Them a Reality

Launching a Business God's Way

RETURN to ME: Reading With the People of God #16

Contending for the Faith in a Compromised World

More Than a Feeling

Living Large in a Small World: A Look Into Philippians 1

Forever Forward in Hope
