Soma Biblia Kila Siku 04/2020预览

Yesu Kristo ni mmiliki, na ana mamlaka juu ya vitu vyote. Pia Yesu ni mnyenyekevu na ana huruma. Alikubali kuyaendea mateso na kifo ili kutuokoa na utumwa wa dhambi. Tutafakari kwa umakini jambo hili la Yesu kufa kwa ajili yetu. Tuige mfano wa watu siku hiyo walipompa Mungu sifa na utukufu, kwani ndiye Muumba wetu. Ni vema tuachilie maisha yetu na vitu tulivyo navyo kwa Bwana ili atutawale. Kwake Yesu tunajifunza kuwa na moyo wa kujitoa kwa ajili ya wengine.