1
Hesabu 13:30
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Lakini Kalebu akanyamazisha watu mbele ya Musa, akasema: Tuende mara moja tuitwae inchi hiyo. Kwa sababu tuko na uwezo sana wa kushinda.
Муқоиса
Hesabu 13:30 омӯзед
2
Hesabu 13:33
Tuliona majitu huko, wazao wa Anaki. Sisi tulijiona kuwa kama mapanzi mbele yao, na ndivyo walivyotuona sisi.
Hesabu 13:33 омӯзед
3
Hesabu 13:31
Lakini watu walioandamana naye kupeleleza inchi wakasema: Hatutaweza kupigana na watu hao; wao wana nguvu kuliko sisi.
Hesabu 13:31 омӯзед
4
Hesabu 13:32
Kwa hiyo wakaeneza mambo ya uongo kati ya watu wa Israeli juu ya inchi waliyoipeleleza, wakisema: Inchi hiyo inawaua watu wake. Vilevile watu wote tuliowaona huko ni wakubwa sana.
Hesabu 13:32 омӯзед
5
Hesabu 13:27
Wakamwambia Musa: Tuliifikia inchi uliyotutuma tuipeleleze; hiyo ni inchi inayotiririka maziwa na asali, na hili ni tunda lake.
Hesabu 13:27 омӯзед
6
Hesabu 13:28
Lakini wenyeji wake ni wenye nguvu sana, na miji yao ni imara na mikubwa sana. Zaidi ya hayo, huko tuliona wazao wa Anaki.
Hesabu 13:28 омӯзед
7
Hesabu 13:29
Waamaleki wanakaa katika eneo la Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanakaa katika eneo la milima, na Wakanana wanakaa karibu na bahari ya Mediteranea na karibu na kingo za muto Yordani.
Hesabu 13:29 омӯзед
8
Hesabu 13:26
Wakawaendea Musa, Haruni na Waisraeli wote pamoja kule Kadesi, katika jangwa la Parani, wakatoa habari ya mambo waliyoona na kuwaonyesha matunda ya inchi.
Hesabu 13:26 омӯзед
Асосӣ
Китоби Муқаддас
Нақшаҳо
Видео