1
Kutoka 5:1
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”
Муқоиса
Kutoka 5:1 омӯзед
2
Kutoka 5:23
Tangu nilipokwenda na kuongea na mufalme wa Misri kwa jina lako, yeye amewatendea watu hawa uovu. Wewe haujafanya lolote kwa kuwakomboa watu wako.”
Kutoka 5:23 омӯзед
3
Kutoka 5:22
Kisha Musa akamugeukia tena Yawe, akasema: “Ee Yawe, kwa nini unawatendea watu hawa uovu? Kwa nini hata ulinituma?
Kutoka 5:22 омӯзед
4
Kutoka 5:2
Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”
Kutoka 5:2 омӯзед
5
Kutoka 5:8-9
Lakini hesabu ya matofali yanayotengenezwa kila siku ikuwe ileile, wala kusipunguke hata tofali moja, kwa sababu watu hawa ni wavivu ndio maana wanapiga kelele na kusema: ‘Utuache tuende kutoa sadaka kwa Mungu wetu.’ Muwazidishie watu hawa kazi ngumu kusudi watoke jasho na kuacha kusema maneno ya uongo.”
Kutoka 5:8-9 омӯзед
Асосӣ
Китоби Муқаддас
Нақшаҳо
Видео