Zaburi 119:81-82
Zaburi 119:81-82 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelingojea neno lako. Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nisemapo, Lini utakaponifariji?
Zaburi 119:81-82 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)
Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako. Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifariji lini?”
Zaburi 119:81-82 Biblia Habari Njema (BHN)
Niko hoi kwa kukungojea uniokoe; naweka tumaini langu katika neno lako. Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Nauliza: “Utakuja lini kunifariji?”
Zaburi 119:81-82 Biblia Habari Njema (BHN)
Niko hoi kwa kukungojea uniokoe; naweka tumaini langu katika neno lako. Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Nauliza: “Utakuja lini kunifariji?”
Zaburi 119:81-82 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelitumainia neno lako. Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nikisema, Lini utakaponifariji?