Yeremia 51:40-41 - Compare All Versions
Yeremia 51:40-41 BHN (Biblia Habari Njema)
Nitawashusha chini kama kondoo wa kuchinjwa, kama vile kondoo dume na beberu. Ajabu kutekwa kwa Babuloni; mji uliosifika duniani kote umechukuliwa! Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!
Yeremia 51:40-41 SUV (Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia)
Nitawatelemsha kama wana-kondoo machinjoni, kama kondoo waume pamoja na mabeberu. Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa! Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa! Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwa Katikati ya mataifa!
Yeremia 51:40-41 SRUV (Swahili Revised Union Version)
Nitawateremsha kama wana-kondoo machinjoni, kama kondoo dume pamoja na mabeberu. Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa! Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa! Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwa Katikati ya mataifa!
Yeremia 51:40-41 NEN (Neno)
“Nitawateremsha kama wana-kondoo wanaoenda machinjoni, kama kondoo dume na mbuzi. “Tazama jinsi Sheshaki atakavyokamatwa, majivuno ya dunia yote yatakavyonyakuliwa. Babeli atakuwa mwenye hofu kiasi gani kati ya mataifa!