Yeremia 5:29-31
Yeremia 5:29-31 Biblia Habari Njema (BHN)
“Je, nisiwaadhibu kwa mambo haya? Je nitaacha kulipiza kisasi taifa kama hili? Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii: Manabii wanatabiri mambo ya uongo, makuhani nao hutafuta faida yao wenyewe; na watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho utakapofika mtafanyaje?”
Yeremia 5:29-31 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Je! Nisiwapatilize kwa mambo hayo? Asema BWANA; na nafsi yangu, je! Nisijilipizie kisasi juu ya taifa la namna hii? Jambo la ajabu, la kuchukiza, limetokea katika nchi hii! Manabii wanatabiri uongo, na makuhani wanatawala kwa msaada wa hao; na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo. Nanyi mtafanya nini mwisho wake?
Yeremia 5:29-31 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Je! Nisiwapatilize kwa mambo hayo? Asema BWANA; na nafsi yangu, je! Nisijilipize kisasi juu ya taifa la namna hii? Jambo la ajabu, la kuchukiza, limetokea katika nchi hii! Manabii wanatabiri uongo, na makuhani wanatawala kwa msaada wa hao; na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo. Nanyi mtafanya nini mwisho wake?
Yeremia 5:29-31 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya hili?” asema BWANA. “Je, nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili? “Jambo la kutisha na kushtusha limetokea katika nchi hii: Manabii wanatabiri uongo, makuhani wanatawala kwa mamlaka yao wenyewe, nao watu wangu wanapenda hivyo. Lakini mtafanya nini mwisho wake?