Yeremia 51:46-47 BHN
Msife moyo wala msiwe na hofu,
kwa sababu ya uvumi mnaosikia nchini.
Mwaka huu kuna uvumi huu,
mwaka mwingine uvumi mwingine;
uvumi wa ukatili katika nchi,
mtawala mmoja dhidi ya mtawala mwingine.
Kweli siku zaja,
nitakapoadhibu sanamu za Babuloni;
nchi yake yote itatiwa aibu,
watu wake wote watauawa humohumo.