Yeremia 51:31-33
Yeremia 51:31-33 BHN
Tarishi baada ya tarishi wanapiga mbio, mjumbe mmoja anamfuata mjumbe mwingine, kumpasha habari mfalme wa Babuloni kwamba mji wake umevamiwa kila upande. Vivuko vya mto vimetekwa, ngome zimechomwa moto, askari wamekumbwa na hofu. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi: “Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafaka wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.”

