Zaburi 119:53-56
Zaburi 119:53-56 SRUV
Ghadhabu kuu imenishika kwa sababu ya wasio haki, Waiachao sheria yako. Amri zako zimekuwa nyimbo zangu, Katika nyumba yangu ya ugenini. Wakati wa usiku nimelikumbuka jina lako, Ee BWANA, nikaitii sheria yako. Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako.