Zaburi 119:53-56
Zaburi 119:53-56 NENO
Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako. Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi. Ee Mwenyezi Mungu, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako. Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.