Zaburi 111
111
Zaburi 111#111 Zaburi hii imetungwa kila mstari ukianzia na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22.
Sifa za Bwana kwa matendo ya ajabu
1 Msifuni Bwana.#111:1 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.
Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote,
katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
2 Kazi za Bwana ni kuu,
wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
3 Kazi zake zimejaa fahari na utukufu,
haki yake hudumu daima.
4 Amefanya maajabu yake yakumbukwe,
Bwana ni mwenye neema na huruma.
5 Huwapa chakula wale wanaomcha,
hulikumbuka agano lake milele.
6 Amewaonesha watu wake uwezo wa kazi zake,
akiwapa nchi za mataifa mengine.
7 Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki,
mausia yake yote ni ya kuaminika.
8 Zinadumu milele na milele,
zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
9 Aliwapa watu wake ukombozi,
aliamuru agano lake milele:
jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
10 Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima,
wote wanaozifuata amri zake wana busara.
Sifa zake zadumu milele.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 111: NEN
Kuonyesha
Nakili
Linganisha
Shirikisha
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.