1
Mattayo MT. 23:11
New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921
SWZZB1921
Nae aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.
Yenzanisa
Ongorora {{vhesi}}
2
Mattayo MT. 23:12
Na ye yote atakaejikuza, atadhiliwa; na ye yote atakaejidhili, atakuzwa.
3
Mattayo MT. 23:23
Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa kuwa mnalipa zaka za mnaana na bizari na kumini, mkaacha mambo makuu ya sharia, hukumu, na rehema, na imani: haya imewapasa kuyafanya, na mengine yale msiyaache.
4
Mattayo MT. 23:25
Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa kuwa nmasafisha nje ya kikombe na chungu, na ndani yake vimejaa unyangʼanyi na kutoa kuwa na kiasi.
5
Mattayo MT. 23:37
Ee Yerusalemi, Yerusalemi, wenye kuwaua manabii, na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! marra ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mbawa zake, wala hamkukubali!
6
Mattayo MT. 23:28
Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, hali kwa ndani mmejaa unafiki na maasi.