Zaburi 114
114
Zaburi 114
Maajabu ya Mungu wakati Israeli walitoka Misri
1 Israeli alipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3 Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.
Selectat acum:
Zaburi 114: NEN
Evidențiere
Copiază
Compară
Împărtășește
Dorești să ai evidențierile salvate pe toate dispozitivele? Înscrie-te sau conectează-te
Holy Bible, Kiswahili Contemporary Version™ (Neno: Biblia Takatifu™) | Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.
Biblica® Cross Reference System | Copyright © 2025 by Biblica, Inc. | Used with permission. All rights reserved worldwide.