Soma Biblia Kila Siku 09/2020Sample

Ezekieli anaelezea kuwa Mungu atakapoamua kuadhibu waliomwasi, hakuna atakayeweza kuiepuka ghadhabu hiyo (m.47-48, Tazama nitawasha moto ndani yako, nao utakula kila mti mbichi ndani yako, na kila mti mkavu; miali ya moto ule haitazimika, na nyuso zote toka kusini hata kaskazini zitateketezwa kwa moto huo. Na watu wote wenye mwili wataona ya kuwa mimi, Bwana, nimeuwasha; hautazimika). Ikumbukwe kuwa siku zote BWANA MUNGU anachukia uovu, na kila tutendapo uovu tunasababisha ghadhabu yake kuwaka juu yetu. Hata hivyo yeye ni mwingi wa rehema, anatualika kutubu.Ugua, basi, Ee mwanadamu; kwa kuvunjika kwake viuno vyako, na kwa uchungu, utaugua mbele ya macho yao(m.6). Hivyo msomaji wa somo hili leo, usifanye moyo wako kuwa mgumu. Jitafakari juu ya mahusiano yako na Mungu, kisha tafuta kutubu na kuanza maisha mapya yapatanayo na toba.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 09/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 2 Wakorintho na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Even in the Shadows: Living With Depression

Marry Me

Deep Roots, Steady Faith

The Invitation of Christmas

Real. Loved. Strengthened: 7 Days With God

Where Are You? A Theology of Suffering

Parenting Through God’s Lens: Seeing Your Child the Way God Does

The Father Lens: Helping Your Kids See Who God Is Through Who You Are

The Single Season
