Soma Biblia Kila Siku 09/2020Sample

Mungu ni mwenye rehema na yupo tayari kuwasamehe wale wote wanaotubu. Lakini bado anabaki na ghadhabu juu ya wale wasiotaka kutubu. Nami nitawasafisha kwa kuwatoa waasi, na hao walionikosa; nitawatoa katika nchi wanayokaa ugenini, lakini hawataingia katika nchi ya Israeli; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana(m.38). Mungu halazimishi watu kumwabudu, ila anatoa fursa kwa kila anayetaka uzima wa milele kumsikiliza na kumfuata. Aidha anawaalika watu wote kumwabudu katika roho na kweli. Kwa maana katika mlima wangu mtakatifu, katika mlima mrefu sana wa Israeli, asema Bwana MUNGU, ndiko watakakonitumikia nyumba yote ya Israeli, wote pia katika nchi ile; nami nitawatakabali huko, na huko nitataka matoleo yenu, na malimbuko ya dhabihu zenu, pamoja na vitu vyenu vitakatifu vyote(m.40). Naye anaahidi kuwabariki wale walio tayari kumwabudu. Mpendwa msomaji, tamani kumwabudu Mungu, kuisikiliza sauti yake na kuyaishi maagizo yake.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 09/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 2 Wakorintho na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Even in the Shadows: Living With Depression

Marry Me

Deep Roots, Steady Faith

The Invitation of Christmas

Real. Loved. Strengthened: 7 Days With God

Where Are You? A Theology of Suffering

Parenting Through God’s Lens: Seeing Your Child the Way God Does

The Father Lens: Helping Your Kids See Who God Is Through Who You Are

The Single Season
