YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku 10Sample

Soma Biblia Kila Siku 10

DAY 27 OF 31

Kufanikiwa kuna hatari, nayo ni kiburi! Tazama m.6 ambapo Mwimba Zaburi anasema kama mpumbavu:Nilipofanikiwa nalisema, Sitaondoshwa milele(ling. Zab 10:6 ambapo mtu anasema vivyo hivyo:Sitaondoshwa, kizazi baada ya kizazi sitakuwamo taabuni). Kwa hiyo akapatwa na hasira ya Mungu, akataka kufa. Lakini akagundua kuwa hasira ya Mungu kwa watu wake ni ya kitambo, yaani, inadumu mpaka tuombe radhi kwake:Ghadhabu zake ni za kitambo kidogo, katika radhi yake mna uhai(m.5). Je, unajua kuwa tunaishi kwa sababu Mungu anatulinda na kutuepusha na kifo? Au kwamba kama tukifanikiwa na kuinuliwa katika maisha, ni kwa sababu ya wema wa Mungu? Tumshukuru Mungu kwa mema mengi tupatayo maishani ili tusijivune na kufa!