YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku 10Sample

Soma Biblia Kila Siku 10

DAY 20 OF 31

Malaika wanapewa wito na Mwimba Zaburi kumwabudu Bwana, na kulisifu jina lake kwa kuwa uwezo wake ni mkuu. Uwezo wake huo umedhihirishwa na sauti yake itendayo maajabu. Ina nguvu ya kupiga kama radi na hata kuivunjavunja mierezi ya Lebanoni. Huleta uhai na kusababisha waabuduo katika hekalu la Mungu kuona utukufu wa Bwana (m.3-9). Naam, na uumbaji wote hutegemea Neno lake, maana Mungu alisema viwepo, vikawa. Zaburi inatukumbusha jinsi Mungu alivyoumba ulimwengu, k.m. Mwa 1:3 ilipoandikwa: Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu yu mfalme milele, na anastahili kuabudiwa. Heri wale ambao nguvu yao ni Bwana!