Soma Biblia Kila Siku 10Sample

Maana ya mstari wa kwanza unaonekana vizuri zaidi katika Kiswahili cha kisasa (Habari Njema): Sasa, kwa vile tumefanywa kuwa waadilifu kwa imani, basi tunayoamani naye Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.Ndugu msomaji, naomba habari hii njema uipokee ipate kukufariji! Kushinda kwako katika hukumu ya Mungu siku ya mwisho kunategemea Yesu Kristo peke yakewala hakutegemei tendo lo lote kwako. Huna sababu ya kuhofu unapomwamini Yesu, maana amani na Mungu umepata bure kwa neema kwa njia ya Yesu Kristo! Zingatia m.2 na m.9-10: Kwa yeye [Yesu Kristo] tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo mnasimama ndani yake; na kufurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu. ...Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. Kwa maana ikiwa tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana baada ya kupatanishwa tutaokolewa katika uzima wake.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.
More
Related Plans

When Your Child Fails: Turning Your Child’s Mistakes Into Moments of Grace and Growth

Always Performing? Even in Your Faith...

Ruins to Royalty

Audacious Faith: Standing Firm in the Fire

Raising Emotionally Resilient Children - Helping Your Child Handle Emotions, Failure, and Pressure With Faith and Strength

A Christian Christmas

Forecast & Focus

The Advent of HOPE and the Object of Our Faith.

LEADERSHIP WISDOM FROM the WILD
