Soma Biblia Kila Siku 10Sample

Yonathani alifanya kazi nzuri ya upatanishaji kati ya baba yake Mfalme na rafiki yake Daudi! Alimhakikishia Sauli kwamba hakuna sababu ya kumchukia Daudi. Ndipo Daudi akarudi kukaa karibu na mfalme. Katika hili Yonathani ni mfano mzuri kwetu Wakristo. Yesu ametuambia: Heri wapatanishi; maana hao wataitwa wana wa Mungu (Mt 5:9). Mkristo wa kweli hapendi ugomvi, bali hutafuta amani. Anajitahidi kuwa mpatanishi kati ya watu kwa maneno na kwa matendo. Maana ana roho ya Mungu, Baba yake, ndani yake! Jinsi hiyo inavyoonekana katika maisha yake, unaweza kusoma katika Rum 12:14-21.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.
More
Related Plans

Finding Joy

Elijah: A Man Surrendered to God

And He Dwelt

The Layoff Test: Trusting God Through a Season of Unemployment

The Power of Biblical Meditation

Joyfully Expecting!

Between the Altar and the Father’s Embrace

Mom in the Word: One-Year Bible Plan (Volume 1)

God’s Word, Her Mission: Encouragement for Women Helping Build God’s Kingdom by Wycliffe Bible Translators
