Soma Biblia Kila Siku 10Sample

Naye Sauli akamwoza Mikali, binti yake. Sauli akaona na kutambua ya kwamba Bwana alikuwa pamoja na Daudi; na huyo Mikali, binti Sauli, akampenda. Naye Sauli akazidi kumwogopa Daudi; Sauli akawa adui yake Daudi siku zote (m.27-29). Ilikuwa ni ahadi ya mfalme kwamba mtu yule atakayemwua Goliathi atapewa binti wa mfalme kama mke wake. Ila binti wa kwanza wa mfalme alishaolewa na mtu mwingine:Ikawa, wakati ule, ilipopasa Daudi apewe Merabu, binti Sauli, aliolewa na Adrieli, Mmeholathi (m.19). Hii ilikuwa ni bahati yake Daudi, maana binti wa pili wa mfalme, Mikali, ndiye aliyempenda (m.20)! Upendo wake huu alionyesha wazi kwa vitendo wakati Sauli, baba yake, alipotaka kumwua Daudi: Kisha Sauli akatuma wajumbe mpaka nyumbani kwa Daudi, ili wamvizie na kumwua asubuhi; naye Mikali, mkewe Daudi, akamwambia, akasema, Wewe usipojiponya nafsi yako usiku huu, kesho utauawa. Basi Mikali akamtelemsha Daudi dirishani; naye akaenda akakimbia na kuokoka(19:11-12).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.
More
Related Plans

Finding Joy

Elijah: A Man Surrendered to God

And He Dwelt

The Layoff Test: Trusting God Through a Season of Unemployment

The Power of Biblical Meditation

Joyfully Expecting!

Between the Altar and the Father’s Embrace

Mom in the Word: One-Year Bible Plan (Volume 1)

God’s Word, Her Mission: Encouragement for Women Helping Build God’s Kingdom by Wycliffe Bible Translators
