1
Mathayo 7:7
Biblia Habari Njema
BHN
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni mlango, nanyi mtafunguliwa.
Compare
Mathayo 7:7ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
2
Mathayo 7:8
Maana, yeyote aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye mlango hufunguliwa.
Mathayo 7:8ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
3
Mathayo 7:24
“Kwa hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
Mathayo 7:24ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
4
Mathayo 7:12
“Yote mnayotaka watu wawatendee nyinyi, watendeeni wao vivyo hivyo. Hii ndiyo maana ya sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.
Mathayo 7:12ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
5
Mathayo 7:14
Lakini njia inayoongoza kwenye uhai ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.
Mathayo 7:14ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
6
Mathayo 7:13
“Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.
Mathayo 7:13ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
7
Mathayo 7:11
Kama basi nyinyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: Atawapa mema wale wanaomwomba.
Mathayo 7:11ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
8
Mathayo 7:1-2
“Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu; kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.
Mathayo 7:1-2ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
9
Mathayo 7:26
“Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
Mathayo 7:26ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
10
Mathayo 7:3-4
Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako? Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako,’ wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?
Mathayo 7:3-4ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
11
Mathayo 7:15-16
“Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!
Mathayo 7:15-16ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
12
Mathayo 7:17
Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
Mathayo 7:17ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
13
Mathayo 7:18
Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
Mathayo 7:18ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ
14
Mathayo 7:19
Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.
Mathayo 7:19ਪੜਚੋਲ ਕਰੋ