1
Rom 8:28
BIBLIA Yenye Vitabu vya Deuterokanoni HABARI NJEMA
SCLDC10
Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kadiri ya kusudi lake.
비교
Rom 8:28 살펴보기
2
Rom 8:38-39
Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: Wala kifo, wala uhai; wala malaika au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka; wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Rom 8:38-39 살펴보기
3
Rom 8:26
Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
Rom 8:26 살펴보기
4
Rom 8:31
Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
Rom 8:31 살펴보기
5
Rom 8:1
Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
Rom 8:1 살펴보기
6
Rom 8:6
Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uhai na amani.
Rom 8:6 살펴보기
7
Rom 8:37
Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
Rom 8:37 살펴보기
8
Rom 8:18
Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyalinganisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
Rom 8:18 살펴보기
9
Rom 8:35
Ni nani awezaye kututenga na upendo wa Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kifo?
Rom 8:35 살펴보기
10
Rom 8:27
Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
Rom 8:27 살펴보기
11
Rom 8:14
Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
Rom 8:14 살펴보기
12
Rom 8:5
Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
Rom 8:5 살펴보기
13
Rom 8:32
Mungu hakumhurumia hata Mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
Rom 8:32 살펴보기
14
Rom 8:16-17
Naye Roho mwenyewe anathibitisha na roho zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
Rom 8:16-17 살펴보기
15
Rom 8:7
Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
Rom 8:7 살펴보기
16
Rom 8:19
Viumbe vyote vinangojea kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
Rom 8:19 살펴보기
17
Rom 8:22
Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
Rom 8:22 살펴보기