Kutoka 10:21-23
Kutoka 10:21-23 SWC02
Yawe akamwambia Musa: “Nyoosha mukono wako juu mbinguni kusudi giza nzito litokee katika inchi ya Misri, giza nzito sana ambalo mutu ataweza kulipapasa.” Basi, Musa akanyoosha mukono wake juu mbinguni, kukakuwa giza nzito katika inchi yote ya Misri kwa muda wa siku tatu. Watu hawakuweza kuonana wala kuondoka pahali walipokuwa kwa muda ule wa siku tatu. Lakini Waisraeli wote walikuwa na mwangaza kule Goseni walikokuwa wanakaa.

