1
Waamuzi 7:2
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Yawe akamwambia Gideoni: “Watu unaokuwa nao ni wengi sana kwangu mimi kwa kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Waisraeli wasipate kujisifu mbele yangu na kusema kwamba wamejiokoa kwa nguvu zao wenyewe.
Lee anya n'etiti ihe abụọ
Nyochaa Waamuzi 7:2
2
Waamuzi 7:7
Yawe akamwambia Gideoni: “Kwa hao watu mia tatu waliokunywa kwa kulamba kama imbwa, nitawaokoa Waisraeli na kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Lakini wale wengine wote warudie kwao.”
Nyochaa Waamuzi 7:7
3
Waamuzi 7:3
Sasa uwatangazie watu wote kwamba mutu yeyote anayekuwa mwoga au anayetetemeka arudi kwake.” Basi, Gideoni akawajaribu, na watu elfu makumi mbili na mbili wakarudi kwao, akabaki na watu elfu kumi.
Nyochaa Waamuzi 7:3
4
Waamuzi 7:4
Yawe akamwambia Gideoni: “Watu hao wangali wengi sana. Sasa uwapeleke kwenye muto, nami nitawajaribu kule. Mutu yeyote nitakayekuambia: ‘Huyu atakwenda nawe, huyo aende nawe. Lakini mutu yeyote nitakayekuambia hatakwenda nawe, huyo asiende nawe.’ ”
Nyochaa Waamuzi 7:4
5
Waamuzi 7:5-6
Basi, Gideoni akawapeleka watu kwenye muto na Yawe akamwambia: “Watu watakaolamba maji kwa ulimi kama imbwa, utawatenganisha na wale watakaopiga magoti kwa kunywa maji.” Jumla ya waliokunywa maji kwa kuchota kwa mikono yao na kulamba kama imbwa ilikuwa mia tatu. Lakini wengine wote waliobaki walipiga magoti kwa kunywa maji.
Nyochaa Waamuzi 7:5-6