YouVersion Logo
Search Icon

Zab 1

1
KITABU CHA KWANZA
Njia Mbili
1 # Mwa 5:24; Ayu 31:5; Zab 81:12; Mit 4:14 Heri mtu yule asiyekwenda
Katika shauri la wasio haki;
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
2Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
3 # Yer 17:8; Mwa 39:3; Zab 128:2 Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji,
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa.
4Sivyo walivyo wasio haki;
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,
Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
6 # Nah 1:7; Yn 10:14 Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea.

Currently Selected:

Zab 1: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy