1 Samueli 10:13-14
1 Samueli 10:13-14 BHN
Shauli alipomaliza kutabiri, alikwenda mahali pa ibada juu. Baba mdogo wa Shauli alipowaona Shauli na mtumishi, akawauliza, “Mlikuwa wapi?” Shauli akajibu, “Tulikwenda kuwatafuta punda, na tulipoona hawapatikani, tulikwenda kumwona Samueli.”