Walawi 19
19
Kutenda mema
1Yawe akamwambia Musa: 2Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu. #Ang. Law 11.44-45; 1 Pet 1.16 3Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu. 4Musigeukie sanamu za miungu, wala musijitengenezee sanamu za kuyeyushwa za miungu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
5Munaponitolea mimi Yawe sadaka za amani, mutanitolea kama vile inavyotakiwa kusudi mupate kukubaliwa. 6Sadaka hiyo inapaswa kuliwa siku hiyohiyo inapotolewa au kesho yake. Chochote kinachobaki mpaka kwa siku ya tatu kinapaswa kuteketezwa kwa moto. 7Kama sehemu ya nyama yake ikikuliwa siku ya tatu, tendo hilo ni chukizo na sadaka hiyo haitakubaliwa. 8Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.
9Utakapovuna mavuno ya inchi yako, usivune kabisa mpaka kwenye mupaka wa shamba wala usirudi nyuma kukusanya mabaki. #Ang. Law 23.22; Kumb 24.19-22 10Musirudie kukusanya kila kitu katika shamba la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini. Utawaachia wamasikini na wageni. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
11Musiibe, musidanganye wala kuambiana uongo. #Ang. Kut 20.15-16; Kumb 5.19-20; Ang. Kut 20.7; Kumb 5.11; Mat 5.33 12Musiape uongo kwa jina langu na kuchafua jina la Mungu wenu. Mimi ni Yawe.
13Usimutese mwenzako wala kumwibia. Usikae na mushahara wa mutumishi wako usiku kucha mpaka asubui. #Ang. Kumb 24.14-15 14Usimulaani kiziwi wala kuweka kizuizi mbele ya kipofu, lakini umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe. #Ang. Kumb 27.18
15Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki. #Ang. Kut 23.6-8; Kumb 16.19 16Usipitepite hata kidogo ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usitie maisha ya mwenzako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ni Yawe.
17Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi. #Ang. Mat 18.15 18Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe. #Ang. Mat 5.43
19Unapaswa kuyashika masharti yangu. Usiiache mifugo yako ipandiwe na nyama wa aina nyingine. Usipande mbegu za aina mbili katika shamba lako. Usivae nguo iliyofumwa kwa aina mbili za nguo. #Ang. Kumb 22.9-11
20Mwanaume akilala na mwanamuke mujakazi ambaye amechumbiwa na mwanaume mwingine, lakini bado hajakombolewa wala kupewa uhuru, uchunguzi ufanywe. Lakini wasiuawe kwa sababu mwanamuke huyo hakukuwa bado huru. 21Mwanaume huyo ataleta mbele ya hema la mukutano sadaka yake ya kondoo dume kwa ajili ya kosa na kunitolea mimi Yawe. 22Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kutumia kondoo huyo mbele ya Yawe kwa ajili ya zambi aliyotenda, naye atasamehewa zambi hiyo aliyotenda.
23Mutakapofika katika inchi ya Kanana na kupanda aina zote za miti ya matunda, matunda hayo hamutayakula. Hamutaruhusiwa kuyakula kwa muda wa miaka mitatu. 24Katika mwaka wa ine matunda yake yote yatakuwa matakatifu, yatatolewa kuwa sadaka ya sifa,#19.24 sifa: au: shukrani. kwa Yawe. 25Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo munaweza kuyakula na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
26Musikule nyama yoyote pamoja na damu. Musifanye ulozi wala kuaguza. #Ang. Mwa 9.4; Law 7.26-27; 17.10-14; Kumb 12.16,23; 15.23; 18.10 27Musikate kwa kiviringo nywele za pembeni ya kichwa wala kunyoa pembe za ndevu zenu. #Ang. Law 2.5; Kumb 14.1 28Musijitie chanjo juu ya mwili wenu kwa ajili ya kuomboleza au kujikatakata chanjo yoyote juu ya mwili. Mimi ni Yawe.
29Usimuchafue binti yako kwa kumufanya kahaba, inchi nzima isipate kuangukia katika ukahaba na hivyo kujaa uovu. #Ang. Kumb 23.17 30Mutashika Sabato zangu na kuheshimu Pahali pangu Patakatifu. Mimi ni Yawe. #Ang. Law 26.2
31Musiwaendee waaguzi wa mizimu wala wachawi kwa kuwaomba wawaaguzie. Mukifanya hivi, mutajichafua. Mimi ni Yawe, Mungu wenu. #Ang. Kumb 18.11; 1 Sam 28.3; 2 Fal 23.4; Isa 8.19
32Unapokuwa mbele ya muzee unapaswa kusimama kwa kumupa heshima yake, nawe umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe.
33Kama kuna mugeni katika inchi yako usimutendee vibaya. #Ang. Kut 22.21; Kumb 24.14-18; 27.19 34Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
35Usikose kuamua kwa haki juu ya vipimo vya urefu, uzito na ujazo. #Ang. Kumb 25.13-16; Mez 20.10; Eze 45.10 36Munapaswa kutumia mizani ya kweli na vipimo vinavyokuwa vya kweli. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri. 37Munapaswa kushika na kutimiza masharti yangu na maagizo yangu. Mimi ni Yawe.
Currently Selected:
Walawi 19: SWC02
Highlight
Share
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Walawi 19
19
Kutenda mema
1Yawe akamwambia Musa: 2Uwaambie Waisraeli wote pamoja hivi: Mukuwe watakatifu maana mimi Yawe, Mungu wenu, ni mutakatifu. #Ang. Law 11.44-45; 1 Pet 1.16 3Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu. 4Musigeukie sanamu za miungu, wala musijitengenezee sanamu za kuyeyushwa za miungu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
5Munaponitolea mimi Yawe sadaka za amani, mutanitolea kama vile inavyotakiwa kusudi mupate kukubaliwa. 6Sadaka hiyo inapaswa kuliwa siku hiyohiyo inapotolewa au kesho yake. Chochote kinachobaki mpaka kwa siku ya tatu kinapaswa kuteketezwa kwa moto. 7Kama sehemu ya nyama yake ikikuliwa siku ya tatu, tendo hilo ni chukizo na sadaka hiyo haitakubaliwa. 8Naye atakayekula nyama hiyo anapaswa kubeba lazima ya uovu wake kwa sababu amechafua kitu kitakatifu cha Yawe. Mutu huyo atatengwa na watu wake.
9Utakapovuna mavuno ya inchi yako, usivune kabisa mpaka kwenye mupaka wa shamba wala usirudi nyuma kukusanya mabaki. #Ang. Law 23.22; Kumb 24.19-22 10Musirudie kukusanya kila kitu katika shamba la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini. Utawaachia wamasikini na wageni. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
11Musiibe, musidanganye wala kuambiana uongo. #Ang. Kut 20.15-16; Kumb 5.19-20; Ang. Kut 20.7; Kumb 5.11; Mat 5.33 12Musiape uongo kwa jina langu na kuchafua jina la Mungu wenu. Mimi ni Yawe.
13Usimutese mwenzako wala kumwibia. Usikae na mushahara wa mutumishi wako usiku kucha mpaka asubui. #Ang. Kumb 24.14-15 14Usimulaani kiziwi wala kuweka kizuizi mbele ya kipofu, lakini umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe. #Ang. Kumb 27.18
15Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki. #Ang. Kut 23.6-8; Kumb 16.19 16Usipitepite hata kidogo ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usitie maisha ya mwenzako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ni Yawe.
17Usimuchukie ndugu yako ndani ya moyo wako, lakini upatane siku zote na mwenzako kusudi usitende zambi. #Ang. Mat 18.15 18Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe. #Ang. Mat 5.43
19Unapaswa kuyashika masharti yangu. Usiiache mifugo yako ipandiwe na nyama wa aina nyingine. Usipande mbegu za aina mbili katika shamba lako. Usivae nguo iliyofumwa kwa aina mbili za nguo. #Ang. Kumb 22.9-11
20Mwanaume akilala na mwanamuke mujakazi ambaye amechumbiwa na mwanaume mwingine, lakini bado hajakombolewa wala kupewa uhuru, uchunguzi ufanywe. Lakini wasiuawe kwa sababu mwanamuke huyo hakukuwa bado huru. 21Mwanaume huyo ataleta mbele ya hema la mukutano sadaka yake ya kondoo dume kwa ajili ya kosa na kunitolea mimi Yawe. 22Kuhani atamufanyia ibada ya upatanisho kwa kutumia kondoo huyo mbele ya Yawe kwa ajili ya zambi aliyotenda, naye atasamehewa zambi hiyo aliyotenda.
23Mutakapofika katika inchi ya Kanana na kupanda aina zote za miti ya matunda, matunda hayo hamutayakula. Hamutaruhusiwa kuyakula kwa muda wa miaka mitatu. 24Katika mwaka wa ine matunda yake yote yatakuwa matakatifu, yatatolewa kuwa sadaka ya sifa,#19.24 sifa: au: shukrani. kwa Yawe. 25Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo munaweza kuyakula na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
26Musikule nyama yoyote pamoja na damu. Musifanye ulozi wala kuaguza. #Ang. Mwa 9.4; Law 7.26-27; 17.10-14; Kumb 12.16,23; 15.23; 18.10 27Musikate kwa kiviringo nywele za pembeni ya kichwa wala kunyoa pembe za ndevu zenu. #Ang. Law 2.5; Kumb 14.1 28Musijitie chanjo juu ya mwili wenu kwa ajili ya kuomboleza au kujikatakata chanjo yoyote juu ya mwili. Mimi ni Yawe.
29Usimuchafue binti yako kwa kumufanya kahaba, inchi nzima isipate kuangukia katika ukahaba na hivyo kujaa uovu. #Ang. Kumb 23.17 30Mutashika Sabato zangu na kuheshimu Pahali pangu Patakatifu. Mimi ni Yawe. #Ang. Law 26.2
31Musiwaendee waaguzi wa mizimu wala wachawi kwa kuwaomba wawaaguzie. Mukifanya hivi, mutajichafua. Mimi ni Yawe, Mungu wenu. #Ang. Kumb 18.11; 1 Sam 28.3; 2 Fal 23.4; Isa 8.19
32Unapokuwa mbele ya muzee unapaswa kusimama kwa kumupa heshima yake, nawe umwogope Mungu wako. Mimi ni Yawe.
33Kama kuna mugeni katika inchi yako usimutendee vibaya. #Ang. Kut 22.21; Kumb 24.14-18; 27.19 34Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.
35Usikose kuamua kwa haki juu ya vipimo vya urefu, uzito na ujazo. #Ang. Kumb 25.13-16; Mez 20.10; Eze 45.10 36Munapaswa kutumia mizani ya kweli na vipimo vinavyokuwa vya kweli. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri. 37Munapaswa kushika na kutimiza masharti yangu na maagizo yangu. Mimi ni Yawe.
Currently Selected:
:
Highlight
Share
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.