Yoshua 16
16
Inchi ya Efuraimu na ya Manase
1Sehemu wazao wa Yosefu waliyogawanyiwa kwa kura ilianzia karibu na muto Yordani, upande wa mashariki wa chemichemi ya Yeriko, na kupitia katika jangwa, hata kwenye sehemu za milima mpaka Beteli. 2Kutoka Beteli, mupaka ulielekea Luzi ukapita Ataroti ambako Waarki waliishi. 3Kisha ukashuka upande wa magaribi katika inchi ya Wayefeleti hata Beti-Horoni ya Chini na Gezeri na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. 4Wazao wa Yosefu, ni kusema kabila la Manase na kabila la Efuraimu, walipewa inchi hiyo kuwa urizi wao.
Inchi ya kabila la Efuraimu
5Watu wa kabila la Efuraimu kulingana na jamaa zao walipata sehemu yao ambayo mupaka wake upande wa mashariki ulipita Ataroti-Adari hata Beti-Horoni ya Juu, 6na kuishia bahari ya Mediteranea. Kwa upande wa kaskazini mupaka ulipita Mikimetati na kwa mashariki yake ulizunguka na kuelekea Tanati-Shilo ambako ulipita upande wa mashariki hata Yanoa. 7Kutoka Yanoa ulikwenda hata Ataroti na Nara, hata kufika Yeriko, ambako uliishia katika muto Yordani. 8Kutoka Tapua, mupaka ulikwenda upande wa magaribi hata kijito cha Kana na kuishia bahari ya Mediteranea. Hii ndiyo inchi watu wa kabila la Efuraimu waliyopewa kulingana na jamaa zao, 9pamoja na miji na vijiji ambavyo waliongezewa kutoka kwenye inchi ya kabila la Manase. 10Waefuraimu hawakuwafukuza Wakanana walioishi Gezeri. Wakanana hao waliendelea kukaa kati ya watu wa Efuraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa. #Ang. Amu 1.29
Currently Selected:
Yoshua 16: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.