YouVersion Logo
Search Icon

Mwanzo 1

1
Kuumbwa kwa ulimwengu
1Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.#1.1 Hapo dunia: au: Hapo mwanzo, Mungu alipoumba mbingu na dunia, 2 dunia ilikuwa bila umbo 2Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho wa Mungu#1.2 roho wa Mungu: au: upepo mukubwa. alikuwa akitanda juu ya maji.
3Mungu akasema: “Mwangaza ukuwe.” Mwangaza ukakuwa. 4Mungu akaona kwamba mwangaza ule ni muzuri. Kisha Mungu akatenganisha mwangaza na giza. 5Mwangaza akauita “Muchana” na giza akaliita “Usiku”. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya kwanza.
6Mungu akasema: “Anga likuwe katikati ya maji, litenge maji sehemu mbili.” 7Ikakuwa hivyo. Mungu akafanya anga, akatenga maji yanayokuwa juu ya anga na yale yanayokuwa chini ya anga lile. 8Mungu akaliita anga “Mbingu”. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya pili.
9Mungu akasema: “Maji yanayokuwa chini ya mbingu yakusanyike pahali pamoja, inchi kavu itokee.” Ikakuwa hivyo. 10Mungu akapaita pahali pakavu “Inchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari”. Mungu akaona kwamba ni vizuri.
11Kisha Mungu akasema: “Inchi ioteshe mimea: mimea inayozaa mbegu, na miti inayozaa matunda yenye mbegu za aina yake.” Ikakuwa hivyo. 12Inchi ikaotesha mimea inayozaa mbegu za aina yake, na miti inayozaa matunda yenye mbegu za aina yake. Mungu akaona kwamba ni vizuri. 13Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya tatu.
14Mungu akasema: “Miangaza ikuwe katika anga, itenge muchana na usiku. Ikuwe vitambulisho kwa kuonyesha nyakati, siku na miaka, 15na iangae katika anga na kuangazia dunia.” Ikakuwa hivyo. 16Mungu akafanya miangaza miwili mikubwa: ule mukubwa utawale muchana na ule mudogo utawale usiku. Akafanya nyota vilevile. 17Mungu akaweka miangaza ile katika anga iangazie dunia, 18ipate kutawala muchana na usiku, na kutenga mwangaza na giza. Mungu akaona kwamba ni vizuri. 19Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya ine.
20Mungu akasema: “Maji yajae makundi ya viumbe vyenye uzima. Na ndege waruke katika anga.” 21Mungu akaumba nyama wakubwa sana wa bahari na aina zote za viumbe vyenye uzima vinavyotembea ndani ya maji. Akaumba aina zote za ndege. Mungu akaona kwamba ni vizuri. 22Mungu akavibariki, akasema: “Muzae, muongezeke, mujaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika inchi.” 23Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya tano.
24Mungu akasema: “Inchi itoe aina zote za viumbe vyenye uzima: nyama wa kufugwa, viumbe vinavyotambaa na nyama wa pori wa kila aina.” Ikakuwa hivyo. 25Mungu akafanya aina zote za nyama wa pori, nyama wa kufugwa, na viumbe vinavyotambaa. Mungu akaona kwamba ni vizuri.
26Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.” 27Mungu akaumba mutu kwa mufano wake. Ndiyo, kwa mufano wake Mungu alimwumba. Aliwaumba mwanaume na mwanamuke. #Ang. 5.1-2 28Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”
29Kisha Mungu akasema: “Ninawapa kila mumea katika dunia unaozaa mbegu na kila muti unaozaa matunda yenye mbegu, kwa ajili ya chakula chenu. 30Nao nyama wote katika dunia, ndege wote wa anga, viumbe vyote vinavyotambaa, kila kiumbe chenye uzima, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikakuwa hivyo. 31Mungu akaona kwamba kila kitu alichofanya ni kizuri kabisa. Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya sita.

Currently Selected:

Mwanzo 1: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy