YouVersion Logo
Search Icon

Maombolezo 5

5
Ombi la kuhurumiwa
1Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;
Utazame na kuiona aibu yetu.
2Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;
Na nyumba zetu kuwa mali ya mataifa.
3Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;
Mama zetu wamekuwa kama wajane.
4Tumekunywa maji yetu kwa fedha;
Kuni zetu twauziwa.
5Watufuatiao wako juu ya shingo zetu;
Tumechoka, tusipate pumziko lolote.
6 # Mwa 24:2; Yer 50:15; Hos 12:1 Tumewapa hao Wamisri mkono;
Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.
7 # Yer 16:12; Eze 18:2; Mt 23:32 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;
Na sisi tumeyachukua maovu yao.
8Watumwa wanatutawala;
Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.
9Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;
Kwa sababu ya upanga wa nyikani.
10Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuri;
Kwa sababu ya joto ya njaa ituteketezayo.
11 # Isa 13:16 Wanawake katika Sayuni wanashikwa kwa nguvu;
Na mabikira katika miji ya Yuda.
12Wakuu hutundikwa kwa mikono yao;
Nyuso za wazee hazipewi heshima.
13 # Amu 16:21 Vijana huyachukua mawe ya kusagia;
Na watoto hujikwaa chini ya kuni.
14 # 2 Fal 25:18 Wazee wameacha kwenda langoni;
Na vijana kwenda ngomani.
15Furaha ya mioyo yetu imekoma;
Machezo yetu yamegeuka maombolezo.
16Taji ya kichwa chetu imeanguka;
Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.
17 # Ayu 17:7; Zab 6:7 Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia;
Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.
18Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa,
Mbweha hutembea juu yake.
19Wewe, BWANA, unadumu milele;
Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.
20Mbona watusahau sikuzote;
Na kutuacha muda huu mwingi?
21Ee BWANA, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale.
22Ingawa wewe umetukataa kabisa;
Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.

Currently Selected:

Maombolezo 5: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy