YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 89:1-18

Zaburi 89:1-18 NEN

Nitaimba juu ya upendo mkuu wa BWANA milele; kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako ujulikane kwa vizazi vyote. Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni. Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu, nimemwapia mtumishi wangu Daudi, ‘Nitaimarisha uzao wako milele na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ” Ee BWANA, mbingu zinayasifu maajabu yako, uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu. Kwa kuwa ni nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa na BWANA? Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni aliye kama BWANA? Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana, anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka. Ee BWANA Mwenye Nguvu Zote, ni nani aliye kama wewe? Ee BWANA, wewe ni mwenye nguvu, na uaminifu wako unakuzunguka. Wewe unatawala bahari yenye msukosuko; wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza. Wewe ulimponda Rahabu kama mmojawapo wa waliochinjwa; kwa mkono wako wenye nguvu, uliwatawanya adui zako. Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako, uliuwekea ulimwengu msingi pamoja na vyote vilivyomo. Uliumba kaskazini na kusini; Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha. Mkono wako umejaa uwezo; mkono wako una nguvu, mkono wako wa kuume umetukuzwa. Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi; upendo na uaminifu vinakutangulia. Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe, wanaotembea katika mwanga wa uwepo wako, Ee BWANA. Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa, wanafurahi katika haki yako. Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao, kwa wema wako unatukuza pembe yetu. Naam, ngao yetu ni mali ya BWANA, na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli.

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy