Sadiraki, Mesaki na Abedenego wakamujibu mufalme: Ee Nebukadneza, sisi hatuhitaji kukujibu juu ya jambo hilo. Mungu wetu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Atatuokoa kutoka furu la moto mukali na vilevile kutoka katika mikono yako, ee mufalme. Lakini, hata kama haitafanyika hivyo, ujue wazi, ee mufalme, kwamba sisi hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya zahabu uliyosimamisha.