Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 1

1
KITABU CHA KWANZA
Njia Mbili
1 # Mwa 5:24; Ayu 31:5; Zab 81:12; Mit 4:14 Heri mtu yule asiyekwenda
Katika shauri la wasio haki;
Wala hakusimama katika njia ya wakosaji;
Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
2Bali sheria ya BWANA ndiyo impendezayo,
Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.
3 # Yer 17:8; Mwa 39:3; Zab 128:2 Naye atakuwa kama mti uliopandwa
Kandokando ya vijito vya maji,
Uzaao matunda yake kwa majira yake,
Wala jani lake halinyauki;
Na kila alitendalo litafanikiwa.
4Sivyo walivyo wasio haki;
Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni,
Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki.
6 # Nah 1:7; Yn 10:14 Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki,
Bali njia ya wasio haki itapotea.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 1: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha